KNAPSACK SPRAYER

 DONDOO ZA MATUMIZI SAHIHI YA 'SOLO' ZA KUPIGIA VIWATILIFU SHAMBANI.

🤏Kabla ya Msimu kuanza ni vema kuhakikisha uko na vitendea Kazi Muhimu,Mojawapo ni Bomba lakupulizia Viwatilifu ( Knapsack sprayer.

🤏 Wakati unajiandaa kwenda Kupuliza Viwatilifu,Fanya yafuatayo.

🔹Kagua kifaa Chako 

🔹Kaza Nozo kwa usahihi na funga Nozo kulingana na aina ya kiwatilifu unachoenda Kupuliza . Zipo Nozo kwa Ajili ya Magugu ( Nozo ya Mkato) , Zipo kwa ajili ya Wadudu na viuwakuvu ( Round Nozo) ,Zipo kwa ajili ya Kupuliza kwenye Mimea mirefu kama mbaazi /Miti ( Nozo ya Njano)

🔹Fanya ukaguzi wa Mwendo ( Calibration)  

🔹Kisha Jaza Maji nusu ya Solo lako.

🔹Unapaswa uwe na kindoo kidogo cha shambani,kisha Weka Maji kama Lita 3 hivi kwenye kindoo.

🔹Chukua Kiwatilifu Chako na pima kiwango cha Dawa kisha Weka ndani ya kindoo na chukua Mti kisha koroga mpaka Mchanganyiko wako uchanganyike vema.

🔹Kisha mimina ndani ya Solo,na Tikisa kwa Muda wa Dakika 1 kisha Jazia Maji kwa kiwango kilichobakia na utikise tena...

⚠️Usitumie Mdomo wako kuzibulia Nozo iliyoziba

⚠️Usijaze Maji Kwenye solo kupita kwenye shingo yake ( Pale Palipoandikwa 15ltr,16ltr,au 18ltr au 20ltr) ukizidisha unajiweka katika hatari ya kumwagikiwa na Kiwatilifu.

⚠️ Hakikisha Maji ni Masafi wakati wa kuchanganya.

⚠️Baada ya kumaliza Kupuliza,safisha Solo lako kwa Maji safi kisha liinamishe livuje Maji kisha nenda lakihifadhi stoo.

⚠️Linda Panya asije kulitoboa.



Felicasto Agrocare for Reliable and Sustainable Services 

Previous Post Next Post

Contact Form